Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Hawza, likinukuu Kitengo cha Habari cha Mshauri wa Utamaduni wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Indonesia, kundi la vijana na watu wanaoipenda Iran kutoka Indonesia, katika hatua ya ubunifu na ya hiari, walipamba magari yao binafsi katika baadhi ya miji ya nchi hiyo kwa picha za Kiongozi Shahidi, mashahidi wa Vita Vitakatifu vya Kujihami, pamoja na picha zinazohusiana na uwezo wa kujihami na mashambulizi ya makombora ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, kisha wakayaendesha katika mitaa ya miji hiyo.
Hatua hii ya ubunifu imepata mwitikio mkubwa katika mitandao ya kijamii na miongoni mwa maoni ya umma, na imechukuliwa kuwa ishara ya mshikamano, uungaji mkono na mapenzi ya sehemu ya jamii ya Indonesia kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Msafara wa magari hayo katika mitaa ya miji, mbali na kuwa na umuhimu wa kiishara, pia umechangia kuibuka kwa harakati za kitamaduni na kimedia, na kusababisha mijadala na mazungumzo mbalimbali kuhusu Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, muqawama na maendeleo ya eneo la Mashariki ya Kati miongoni mwa makundi tofauti ya jamii.
Hatua kama hizi za wananchi zinaonyesha kwamba; kuna uwezo mkubwa wa kupanua mahusiano ya kitamaduni na kijamii kati ya mataifa ya Iran na Indonesia, aidha, ikiwa uwezo huo utaelekezwa na kutumiwa ipasavyo, unaweza kutumika katika kuimarisha diplomasia ya umma na ya wananchi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Maoni yako